Skip to main content

KUHUSU MWANDISHI—EMMANUEL KIMANISHA


Emmanuel Kimanisha ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dodoma katika shahada ya kwanza ya ualimu wa sayansi. Yuko mwaka wake wa tatu katika chuo hicho lakini ni mtu mwenye shauku kubwa sana na anayependa kutafuta maarifa ya mambo na vitu mbalimbali ambavyo hutumia muda wake wa ziada kuvifuatilia na kuvifanyia majaribio ya vitendo. Katika kufanya hivyo, anayo shauku kubwa ya kuwa na uwanja mpana zaidi wa kujifunza na kufundisha kwa undani ili kushirikishana maarifa, taarifa na ufahamu wa mambo yote yanayowezekana kueleweka na kufundishika kwake. Miongoni mwa mambo ambayo huyafuatilia kwa muda wake wa ziada ni pamoja na maarifa ya mambo yanayohusu namna ya kutumia fursa mbalimbali zilizopo katika teknolojia ya habari na mawasiliano—intaneti na mengine mengi yanayohusu nadharia za Electronics na Robotics.

Kuna vitabu vyake miongoni mwa vitabu vingine vidogo vidogo ambavyo ameviandika na kuwashirikisha watu mbalimbali, kwa yale ambayo ameyafuatilia na kuyafanyia majaribio ya vitendo. Vitabu hivyo vitakusaidia kupata mwanga mkubwa kwa kuwa na namna nyingine nzuri unayoweza kuutazama mtandao wa intaneti. Ili kupunguza hata kuondoa kabisa watu wanaotumia mtandao wa intaneti chini ya viwango au nje na manufaa stahiki, katika nchi yetu na bara letu la Afrika . 

Intaneti ikitumika kwa uzuri na faida , inaweza kusaidia sana katika kubadilisha maisha yako na ya watu wengine wengi. Utaweza kutambua na kufahamu mambo kadhaa muhimu, ambayo yatakupeleka katika hatua nyingine nzuri ya kutumia intaneti kwa manufaa makubwa zaidi hususan kiuchumi na kijamii. Hata kama haukuwahi kufikiria kutumia intaneti kwa namna yoyote ile kukunufaisha kiuchumi, utaweza kupata mambo yatakayokupa mwanga wa namna ya kuanza. 

Kila mtu anaweza kufanya jambo jema na zuri lenye manufaa makubwa kwake na kwa jamii yake, kupitia intaneti. Na ni vyema kutambua kuwa; kule tunakoelekea kutakuhitaji uwe na jukwaa lako mtandaoni kwa sababu intaneti na Electronics zitachukua nafasi kubwa katika uendeshaji wa mambo mengi katika nyanja zote. Hivyo kujiandaa na kuanza kupata uzoefu ni muhimu mno kuliko vile mtu asiyeona mbali anavyofikiri.

Emmanuel Online Gadgets 77 (EO Gadgets 77) inahusika na mambo makuu matatu; kuandika kazi za maandishi za maelezo ya kawaida kwa kuwahudumia hata watu walio mbali kwa kupitia intaneti (Emmanuel Online Typing and Transcription Gadget 7 (—EOTTG 7), Kubuni na kutengeneza graphics mbalimbali (EO Gadgets 77 Designs) na inatarajia kukamilisha usajili kwa ajili ya shule na maktaba za mtandaoni [Emmanuel Online Schools and Libraries (EOSL)] kwa ajili ya kuendelea kushirikisha maarifa na njia mbadala katika uvumbuzi wa mambo ya teknolojia ya habari na mawasiliano katika intaneti na kwa kugusia nadharia zinazolenga kuonyesha muunganiko unaoelekea kuwepo kati ya intaneti na Electronics (Advanced Electronics and Robotics), ili kukabiliana ipasavyo na wazo lijalo la Intaneti ya Vitu (Internet of Things (IoT)— kutoka katika nchi zilizoendelea, ambalo ni wazo linalokwenda kubadili sura ya intaneti kwa kiasi kikubwa. 

Kwa sasa EO Gadgets 77 inajihusisha zaidi na uandishi wa kazi za maandishi na kisha wateja wake kuzipokea katika fomati za kielektroniki (softcopy) popote walipo —(EOTTG) na pia kwa sehemu inajaribu kufanya utekelezaji wa kushirikisha kwa sehemu; maarifa mbalimbali yanayohusiana na mambo tajwa hapo juu (EOSL) ,kwa njia ya intaneti kupitia Blogu ndogo na Makundi ya Whatsapp.

Emmanuel Kimanisha. 
emmanuellibraries@gmail.com

Comments

Popular posts from this blog

240 WHATSAPP GROUPS' LINKS (Business and Social)—Tanzania.

Tumekukusanyia [links] viunganishi vya vikundi vya WhatsApp zaidi ya 240, vya kibiashara na mambo ya kijamii, vya nchini Tanzania. Utawafikia watu wengi (zaidi ya 43,200) waliopo WhatsApp , kwa urahisi—ndani ya muda mfupi. Ili wafahamishwe kuhusu uwepo wa huduma au biashara yako. Hapa nitakuonyesha orodha ya vikundi 244 vya WhatsApp , ambavyo links zake zipo kwenye dokumenti ya PDF tuliyoiandaa. Tumetengeneza dokumenti ya PDF, ambayo kila jina la kikundi lina link chini yake; ili uweze ku-join kupitia dokumenti ya PDF. Dokumenti inapatikana kwa  TSH 1,500.  Namba yetu ya malipo ni 0743517138—EMMANUEL KIMANISHA. Vikundi vya WhatsApp vilivyomo ni: 1) MADALALI NA WAPANGAJI 2) TAARIFA MUHIMU ZA JAMII 3) DAR FAST DEALS 4) AGIZA NASI CHINA 03 5) BEI NDOGO IRINGA & DAR ES SALAAM 6) THE CITY OF BUSINESS 7) MAPINDUZI UFUGAJI 8) CHAMPION INVESTMENT 9) TEAM CALVO TRIPLE EARN 10) FINANCIO INVESTMENT 11) CHINA SHARE MOQ 12) MUCE, RUCU & TUMAINI (MRT) 13) MAPISHI 14) MARKETING IRING...

EO Gadgets Images

K NEW AND EDITED T

KALENDA NZURI [2021] YENYE PICHA ZAKO.

Ofa nzuri ya muda mfupi; n dani ya siku chache. Baada ya kuona watu wengi wanahitaji kalenda lakini wapo mbali, nimeamua kutoa ofa ya muda mfupi; uweze kupata 'softcopy' (PDF & Picha original ya jpg) ya kalenda yako  ya mwaka 2021 [yenye picha zako] kwa Tsh 2,000 badala ya Tsh 4,500. Tuma tu picha zako hata sasa, unazotaka ziwepo kwenye kalenda; ndani ya dakika chache kalenda itakuwa tayari na kuipata leo leo —kwa wasapu/e-mail. 🗞️📜📲 Bei hii inakupa nafasi nzuri ya kui-print ukiwa mahali popote wanapo-print picha au dokumenti za rangi (stationery/studio ya picha); ni rahisi sana. Ukifika mahali popote wanapofanya hivyo (printing) (stationery au photo studio) unawapatia namba zetu ili kuweka mambo vizuri zaidi —wakati wa 'printing' ya kalenda yako. Tupo na wewe popote. Tupo hewani sasa hivi kwa Whatsapp na mawasiliano ya kawaida. WhatsApp: +255 743 517 138 /call. Ikiwa unatumia wasapu sasa hivi (online); Ingia HAPA [CLICK HERE] kwa ajili ya ...